Search This Blog
Friday, May 31, 2019
Kisa cha Ferooz, Luludiva Kuwasaidia Wahudumu wa Baa
Msanii wa muziki wa bongo fleva Lulu Abbas maarufu kama Luludiva anaetamba na wimbo wa mapopo amesema kwa sasa ameandaa mpango maalumu kwaajili ya mabinti wanaofanya shughuli za uhudumu wa baa
Kwenye mahojiano na dozenselection Luludiva amesema kuwa ameamua kuja na mpango wa kuanzisha Foundation kwaajili ya kuwasaidia wahudumu wa baa hasa mabinti wanaonyanyasika na kudharaulika.
Ameongeza kuwa hata yeye alipitia huko kwani aliwahi kuwa mhudumu wa baa kabla ya kuwa staa wa muziki hivyo anatambua manyayaso, dharau na matusi wanayokumbana nayo wahudumu hao.
Ameongeza kuwa lengo kubwa la kuanzisha foundation hiyo ni kuwapa ushawishi na kuwasaidia pale itakapo wezekana ili waweze kutimiza malengo yao.
Balozi huyo wa Kampuni ya simu ya infinix ameongeza kuwa hakuwahi kulipwa alipokuwa anafanya kazi ya uhudumu wa baa kwa mkongwe wa muziki Ferooz na kwamba alifanya kazi hiyo kwa kudharaulika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment