Search This Blog
Friday, May 24, 2019
DC Muro atimiza ahadi kwa manusura wa ajali ya moto
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Jerry Cornel Muro amekabidhi Mifuko Ishirini ya Saruji ( Cement) ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake ya kuisaidia familia ya Bw Eliud Samwel Nyari ambaye nyumba yake iliungua kwa moto na kusababisha kifo cha mtoto wake wa kike Mercy mwenye umri wa miaka miwili na nusu katika kijiji cha Loita Nkwamala kata ya Nkwandrua Halamashauri ya Meru.
Dc Muro amekabidhi mifuko hiyo 20 kwa mjumbe wa Kamati ya kusaidia kumjengea Nyumba, Ndugu Eliud ambae yeye na familia yake yenye watu saba kwa sasa hawana mahali pa kuishi uku wakiwa na majonzi ya kuondokewa na binti yao mpendwa Mercy aliefariki kwenye ajali ya moto.
Pia Dc Muro ameomba wasamaria wema kusaidia kuchangia vifaa vya ujenzi yakiwemo mabati, nondo na mchanga pamoja na cement ili kuiwezesha familia hiyo kupata sehemu ya kiwasitiri na kuendelea na maisha .
http://bit.ly/2wmZToF
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...
No comments:
Post a Comment