Search This Blog

Thursday, May 23, 2019

BREAKING: Shule ya wasichana Ashira yateketea kwa moto


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mnghwira, ameeleza kuwa amepokea kwa masikitiko ajali ya moto iliyotokea leo Mei 23, kwenye Shule ya Sekondari ya wasichana ya Ashira iliyopo Marangu Mkoani Kilimanjaro.

Mkuu huyo akiongea muda mfupi baada ya moto huo uliounguza mabweni amesema bado hajapata tathmini kamili ya ajali, lakini Kamanda wa Polisi mkoani humo ambaye amewahi eneo la tukio, amemweleza kuna uwezekano mkubwa kuwa hakukuwa na mwanafunzi bwenini.

''Shule ya Ashira ni miongoni mwa shule kongwe ambazo zipo kwenye mpango wa kufanyiwa marekebisho na niliitembelea hivi karibuni, lakini nasikitika leo imeungua upande wa mabweni. Baadaye tutapata tathmini maana Kamanda yupo kule na RAS naye amekwenda'', ameeleza.




http://bit.ly/2X5g7Pa

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...