Search This Blog

Thursday, September 2, 2021

Putin ailaumu Marekani kwa janga la Afghanistan


Rais wa Urusi Vladimir Putin alielezea hali iliyoibuka kama "janga na upotezaji", na Marekani imekuwa ikijaribu kuweka sheria zake na mtindo wa maisha huko Afghanistan kwa miaka 20.

Putin aligusia suala la Afghanistan katika mazungumzo yake na wanafunzi wa jiji la Vladivostok mashariki mwa nchi kwa sababu ya kuanza kwa mwaka mpya wa masomo.

Akikumbusha kwamba vitengo vya jeshi la Marekani vimekuwa katika eneo la Afghanistan kwa miaka 20, Putin alisema kuwa Marekani ilikuwa ikijaribu "kuwastaisha" watu wanaoishi Afghanistan wakati huu.

Putin alisema,

"Marekani kweli ilitaka kupitisha sheria zake, mtindo wa maisha na taasisi za kisiasa nchini Afghanistan kwa maana pana zaidi. Kwa wale wanaofanya hivi, kwa Marekani na kwa wale wanaoishi Afghanistan, matokeo yake ni janga na hasara."

Akieleza kuwa mkasa huu ulitokea kwa sababu historia, utamaduni, falsafa ya maisha ya watu wanaoishi Afghanistan haikuzingatiwa na mila yao wala haikuheshimiwa, Putin aliendelea na maneno yake kama ifuatavyo:

"Inahitajika kuelewa kuwa haiwezekani kulazimisha chochote kutoka nje. Hali lazima ikomae. Ikiwa unataka hali hiyo kukomaa haraka, ni muhimu kusaidia watu. Ndio, inaweza na inapaswa kufanywa kwa namna hii. Lakini ni lazima ifanyike kwa njia ya kistaarabu, kwa uangalifu, kudumisha mwelekeo mzuri, bila haraka na kwa uvumilivu. Bila sababu hizi ni vigumu kufikia chochote.”

 




No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...