Search This Blog

Monday, August 30, 2021

Wezi washambulia gari lililobeba chanjo za Kovid-19 na kuiba dozi 300 Wezi washambulia gari lililobeba chanjo za Kovid-19 na kuiba dozi 300

Gari lililobeba aina mpya ya chanjo ya corona (Kovid-19) lilishambuliwa huko Tehran, mji mkuu wa Iran. Ilitangazwa kuwa watu walioshambulia gari hilo waliiba dozi 300 za chanjo.

Gari lililobeba chanjo za corona lilishambuliwa baada ya kutoka kwenye ghala ya Wizara ya Afya ya Iran katika mkoa wa Yaftabad.

Washambuliaji waliiba dozi 300 za chanjo ya Kovid-19, baada ya kumpiga dereva wa gari.

Habari kwamba chanjo hizo ziliibiwa pia zilithibitishwa na Mkuu wa Polisi wa Tehran Husein Rahimi na Meneja Mkuu wa Mahusiano ya Umma wa Wizara ya Afya Kiyanuş Cihanpur.

Mkuu wa Polisi Rahimi alisema kuwa juhudi zinaendelea kuwakamata wezi hao.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...