Vyama vya upinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo vimeitisha maandamano ya umma mwezi ujao kushinikiza kusawazishwa kwa sheria za uchaguzi.
Upinzani umepinga sheria inayosimamia Tume huru ya Kitaifa ya Uchaguzi (Ceni) na kuonya dhidi ya majaribio yoyote ya kuchelewesha kura ya mwaka wa 2023.
Rais Felix Tshisekedi anatuhumiwa kuzuia mchakato wa uchaguzi wakati wakuu wa madhehebu ya kidini wanahangaika kuafikia makubaliano juu ya mtu mwenye haiba gani anayepaswa kuongoza Ceni.
Viongozi wawili wakuu wa Muungano wa upinzani maarufu Lamuka, Martin Fayulu na Adolphe Muzitois wameitisha maandamano ya Septemba 15 kote nchi.

No comments:
Post a Comment