Search This Blog

Sunday, August 29, 2021

Liverpool yabanwa mbavu dhidi ya Chelsea pungufu

WENYEJI, Liverpool wamelazimishwa sare ya 1-1 na Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku huu Uwanja wa Anfield.

Chelsea ilimaliza pungufu leo baada ya Reece James kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45 na ushei kwa kuunawa mpira kwenye boksi na kusababisha penalti ambayo Mohamed Salah aliifungia Liverpool.

James aliikutwa na majanga hayo baada ya kuisaidia Chelsea kupata bao la kuongoza dakika ya 22 kwa kazi yake nzuri kumaliziwa na mfungaji Kai Havertz na sare hiyo inafanya timu zote zifikishe pointi saba baada ya mechi tatu za mwanzo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...