Search This Blog

Saturday, June 19, 2021

Mhafidhina Ebrahim Rais ashinda uchaguzi wa rais Iran


Wizara ya Mambo ya ndani ya Iran imemtangaza mhafidhina mwenye msimamo mkali Ebrahim Raisi, kuwa mshindi wa urais baada ya kuhesabiwa kwa kura nyingi na wapinzani kukubali kushindwa.Raisi, mtumishi wa kidini mwenye umri wa miaka 60, anaetajwa kuwa karibu sana na kiongozi wa juu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei, atamrithi rais mwenye msimamo wa wastani, Hassan Rouhani. 

Hii itaashiria mabadiliko makubwa katika mwelekeo kwa serikali nchini Iran, baada ya miaka minane chini ya Rouhani. 

Msemaji wa wizara ya mambo ya ndani amesema leo kuwa Raisi amepata kura zisizopungua milioni 17.8, kati ya jumla ya kura milioni 28.6 zilizopigwa siku ya Ijumaa. 

Matokeo ya mwisho yanatarajiwa kutangazwa baadae wikendi hii. 

Ebrahim Raisi ataapishwa mwezi Agosti.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...