Search This Blog

Wednesday, May 26, 2021

Wanaharakati wapinga mifumo ya akili bandia inayowapeleleza watu wa jamii ya Uyghur China


Mfumo wa kamera unaotumia akili bandia na utambuzi wa sura kwa ajili ya kubaini hisia umejaribiwa kwa watu wa jamii ya Uyghur mjini Xinjiang, BBC imeelezwa.

Mhandisi wa Programu amedai kuiweka mifumo hiyo kwenye vituo vya polisi vya jimbo.

Mwanaharakati wa masuala ya kibindamu aliyeoneshwa ushahidi ameeleza kama kitendo cha kushtusha.

Ubalozi wa China nchini Uingereza haujajibu shutuma zilizoelekezwa kwa China lakini umesema kuwa wanahakikisha kuzingatiwa kwa haki za kijamii na kisiasa kwa makundi ya jamii zote.

Xinjiang ni makazi ya jamii ya walio wachache wa Uyghur milioni 12, wengi wao Waislamu.

Raia katika mkoa huo hupelelezwa kila siku. Eneo hilo pia ni makazi ya "vituo vya mafunzo " vilivyosababisha utata, vinaitwa na makundi ya kutetea haki za binadamu kama kambi za kizuizi na ambapo inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni moja wamewekwa katika kambi hizo.

Beijing daima imekuwa ikisema kuwa upelelezi ni muhimu katika eneo hilo kwa sababu inasema jamii hiyo inayotaka ambao kuanzisha jimbo lao wameua mamia ya watu katika mashambulio ya kigaidi.

Mhandisi wa programu hiyo alikubali kuzungumza na kipindi cha BBC cha Panorama bila kutajwa jina, kwa sababu anahofia usalama wake. Kampuni aliyoifanyia kazi pia haijawekwa wazi.

Lakini aliionesha Panorama picha tano za wafungwa wa Uyghur ambao alidai walipimwa kwa mfumo huo wa akili bandia.

"Serikali ya China hutumia watu wa Uyghurs kwa majaribio kama vile panya wanavyotumiwa kwenye maabara," alisema.

Na alielezea jukumu lake katika la kufunga kamera katika vituo vya polisi katika jimbo hilo: "Tuliweka kamera ya kugundua hisia umbali wa mita 3 aliposimama mtu. Ni sawa na kifaa cha kupeleleza kama mtu anasema uongo lakini teknolojia hii ni ya hali ya juu zaidi."

Alisema maafisa walitumia "viti vya kuzuia wafungwa" ambavyo vimewekwa sana katika vituo vya polisi kote China.

"Mikono yako imefungwa mahali na vizuizi vya chuma, na pia vifundo vya miguu."

Alitoa ushahidi wa jinsi mfumo wa akili bandia umefundishwa kugundua na kuchambua hata mabadiliko ya dakika katika sura na vishimo vya ngozi.

Kulingana na madai yake, programu hiyo inaunda chati ya pai, na sehemu nyekundu ikiwakilisha hali hasi ya akili au wasiwasi.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...