Matumaini ya Paris St-Germain na Manchester City kumsaini Lionel Messi yamefufuliwa upya baada ya mgombea urais wa Barcelona Emili Rousaud kusema ''ni vigumu kumudu'' mshahara wa Muargentina huyo baada ya mkataba wake wa sasa kumalizika msimu ujao. (AS - in Spanish)
Rousaud anataka kuwakutanisha Messi na mshambuliaji wa Brazil na Paris St-Germain Neymar Uhispania lakini Barca haina uwezo wa kumudu bei ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 28- kabla ya mkataba wake kumalizika mwaka 2022. (AS - in Spanish)
Mlinzi wa zamani wa Manchester City Pablo Zabaleta amesema klabu hiyo ya Ligi ya Primia ni "mahali pazuri" kwa Messi ikiwa mchezaji huyo ataamua kuondoka Barca. (Stadium Astro, via Sun)
Kuna "uwezekano mkubwa" Messi ataondoka Barca na kujiunga na PSG msimu ujao, huku mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 21, akitarajiwa kijiunga na Real Madrid. (TalkSport)
West Brom wanajiandaa kumfuta mkufunzi wao Slaven Bilic na kumpatia nafasi yake kocha wa zamani wa England Sam Allardyce. (TalkSport)
Bayern Munich wako tayari kumpatia kiungo mshambuliaji wa kati Jamal Musiala, 17, mkataba mpya wa thamani ya £100,000 kwa wiki licha nyota huyo kunyatiwa na klabu za Ligi Kuu ya England. (Mail)
Wakala wa Mesut Ozil amesema kiungo huyo wa kati wa Ujerumani aliye na umri wa miaka 32, anataka kusalia Arsenal kukamilisha miezi sita ya mwisho ya kandarasi yake - Licha ya klabu hiyo kumtaka aondoke mwezi Januari. (Tuttomercato - in Italian)
Arsenal na Marseille wanataka kumsajili kiungo wakati wa Portugal Fabio Vieira, 20, kutoka Porto. (Record - in Portuguese)

No comments:
Post a Comment