Search This Blog

Monday, December 14, 2020

Magaidi 20 wa kundi la Boko Haram wauawa na jeshi la Nigeria


Wanamgambo 20 wa kundi la kigaidi la Boko Haram wameripotiwa kuangamziwa kwenye operesheni iliyofanyika nchini Nigeria.

Kundi hilo la kigaidi la Boko Haram lilikuwa likijaribu kuendesha shambulizi kwenye mkoa wa Askira Uba jimbo la Borno.

Naibu Msemaji wa Kikosi cha Jeshi la Nigeria Ado Isa, alitangaza kuwa shambulizi hilo lilizuiliwa  kutekelezwa, na magaidi 20 waliuawa huku magari 4 ya silaha yaliyomilikiwa na kundi hilo yakikamatwa.

Mwanajeshi 1 alipoteza maisha na wengine 2 wakajeruhiwa katika operesheni hiyo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...