Search This Blog

Tuesday, November 10, 2020

Tetesi za soka kimataifa


 Klabu ya Paris St-Germain itafirikiria kuwasilisha ombi la kumsajili winga wa Juventus Cristiano Ronaldo iwapo klabu hiyo ya Itali itaamua kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35. (Mail)

PSG pia imeanza mazungumzo ya kumpatia kandarasi mpya mshambuliaji wa Brazil Neymar, huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 akifurahia kutia saini kandarasi mpya ya miaka mitano (ESPN)

Arsenal ni miongoni mwa baadhi ya klabu ambazo zinamuwania mshambuliaji wa Sao Paulo na Brazil Brenner, 20. (Calciomercato - in Italian)

Aliyekuwa beki wa Liverpool Jamie Caragher anaamini kwamba Man United inafaa kumuuza kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba 27. (Talksport)

Manchester United huenda ikawasilisha ombi la kumsajili kiungo wa kati wa Aston Villa na England Jack Grealish, 25, iwapo Pogba ataondoka Old Trafford. (Manchester Evening News)

Arsenal ilikaribia kumsaini kiungo wa kati wa Borussia Dortmund Jude Bellingham, 17, kutoka klabu ya Birmingham City 2019. (Sky Sports, via Independent)

The Gunners pia wameanzisha mazungumzo na kiungo wa kati wa Red Bull Salzburg Dominik Szoboszlai, 20. Arsenal inafikiria kuwasilisha ombi la £22m kumnunua mchezaji huyo wa Hungary. (Football London)

Leicester City imefungua mazungumzo kuhusu kandarasi mpya na beki Jonny Evans . Raia huyo wa Ireland Kaskazini 32, anaingia katika mwaka wake wa mwisho wa kandarasi ya miaka mittu alioandikisha.. (Athletic - subscription required)

Kiungo wa kati wa Uholanzi Donny van de Beek, 23, anataka kuichezea zaidi Manchester United lakini huenda akatatizika kuingia katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo , kulingana mkufunzi Frank de Boer. (Sun)

Kiungo wa kati wa Chelsea Danny Drinkwater amechapisha kanda ya video inayomuangazia katika juhudi za kuondoka katika klabu hiyo. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 amekuwa aifanya mazoezi peke yake baada ya kuondolewa katika kikosi cha kwanza katika uwanja wa Stamford Bridge. (Mail)

Winga wa Ivory Coast Nicolas Pepe, 25, amelalamika kuhusu fursa chache anazopewa kushiriki katika mechi katika klabu ya Arsenal. (Canal Plus, via Mirror)

Kipa wa Liverpool na jamhuri ya Ireland kaskazini Caoimhin Kelleher, 21, anataka kuondoka katika klkabu hiyo ka mkpo mwezi Januari iloi kuongeza fursa ya kushiriki katika. (Liverpool Echo)

Mchezaji siye na klabu na kiungoi wa kati wa zamani wa Arsenal Jack Wilshere, 28, anasema kwamba hatoweza kujiunga na Tottenham kutokana na uhusiano wake na The Gunners.. (Goal)

Kiungo wa kati wa Manchester United na England Jesse Lingard, 27, amewacha kufanya kazi na ajenti Mino Raiola. (ESPN)



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...