Search This Blog
Wednesday, November 6, 2019
CHADEMA Walimwa Barua Nyingine na Msajili wa Vyama vya Siasa
Msajili wa vyama vya siasa nchini Tanzania amekiandikia barua Chadema kukitaka kuwasilisha ratiba ya mkutano mkuu wa kuchagua viongozi wa kitaifa wa chama hicho kabla ya Novemba 11, 2019.
Barua hiyo imetolewa Jumatano Novemba 6, 2019 na naibu msajili wa vyama vya siasa, Sisty Nyahoza kwa niaba ya msajili wa vyama vya siasa, Jaji Francis Mutungi.
Oktoba Mosi, 2019 chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania kiliandikiwa barua na ofisi hiyo wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua kwa madai ya kukiuka Sheria ya Vyama vya Siasa kwa kuchelewa kufanya uchaguzi mkuu wa chama hicho.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...


No comments:
Post a Comment